Hali Halisi: Maoni ya wananchi juu ya elimu bila malipo ya ada.
24 Nov 2016
hot
| Machapisho

Kufuatia kuanzishwa kwa mfumo wa elimu bila malipo ya ada, asilimia 50 ya wananchi wanasema ubora wa elimu umeongezeka. Lakini asilimia 35 wanasema ubora wa elimu umebaki palepale huku asilimia 15 wakisema umeshuka.
Matokeo haya yametolewa na Twaweza katika muhtasari wake Hali halisi: Maoni ya wananchi juu ya elimu bila malipo ya ada. Muhtasari huo unatokana na takwimu kutoka Sauti za Wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika wenye uwakilishi wa kitaifa na unaotumia simu za mikononi. Matokeo haya yanatokana na takwimu zilizokusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,806 kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara kati ya tarehe 7 na tarehe 14 agosti 2016. (Zanzibar haihusiki kwenye matokeo haya)
Wananchi wengi wana mitazamo chanya juu ya elimu nchini Tanzania, lakini, ni dhahiri kuwa shule za serikali bado zinakabiliwa na changamoto mbalimbali. Kwa mujibu wa wahojiwa, changamoto kuu ni ukosefu wa walimu (imetajwa na asilimia 34), madawati (asilimia 30) na madarasa (asilimia 13), pamoja na uhaba wa vitabu (asilimia 7).
Endelea kusoma:
Editors: Aidan Eyakuze
pakua nyaraka
- Hali Halisi | Muhtasari | 1.13 MB
- Wananchi wanasema ubora wa elimu umeongezeka tangu kuanzishwa kwa mfumo wa elimu bila malipo ya ada. Lakini Watanzania 6 kati ya 10 wangewapeleka watoto wao shule binafsi kama wangekuwa na uwezo | Taarifa kwa Vyombo vya Habari | 387.47 KB
- Reality Check | Research Brief | 0 Bytes
- 50% think that quality has improved since the introduction of fee free education. At the same time, 6 out of 10 citizens would send their children to private school if they could | Press Release | 393 KB
- Dodoso | 143.48 KB
Tafsiri
unaweza pia kupenda...
- Fedha, fedha, fedha! Wananchi na huduma rasmi za kifedha. (15 Dec 2016)
- Demokrasia, udikteta na maandamano: Wananchi wanasemaje? (28 Sep 2016)
- Rais wa watu? Tathmini na matarajio ya wananchi kwa serikali ya awamu ya tano (14 Sep 2016)
- Je, watoto wetu wanajifunza? (31 Aug 2016)
- Nyota njema huonekana asubuhi: Maoni ya wananchi kuhusu huduma za afya (10 Aug 2016)
- Masuala ya Muungano: Maoni ya wananchi kuhusu kinachoendelea Zanzibar (5 Jul 2016)
- Mwangaza: wananchi na haki ya kupata habari (27 Apr 2016)